Monday, July 6, 2015

AZAM FC KUWEKA KAMBI MIKOANI

Posted By: kj - 3:52 PM

Share

& Comment

Kikosi cha Azam Fc kitakachoshiriki michuano ya Kagame, kinaarajia kuweka kambi mjini Tanga.

Chini ya Muingereza, Stewart Hall kinatarajia kuondoka siku yoyote ndani ya wiki hii kwenda kuweka kambi.

Azam FC ikiwa mjini humo, itapata nafasi ya kucheza mechi za kirafiki kujipima nguvu shisi ya wakongwe African Sports na Coastal Union.

Msemaji wa timu hiyo, Jaffar Idd Maganga, alisema wanaenda kuweka kambi mkoani humo kutokana na maagizo maalumu ya kocha wao ya kutaka kwenda kuweka kambi nje ya Dar.

“Ni kweli kuwa tunaenda kuweka kambi maalumu mkoani Tanga kwa ajili ya kujiweka sawa kabla ya kuanza kwa ligi kuu pamoja na mashindano ya Kagame.

“Kambi hii ni maalumu kutokana na maagizo ya kocha Stewart Hall pamoja na benchi lake la ufundi kuhitaji timu kwenda kuweka kambi nje ya jiji la Dar ambapo tukiwa mkoani humo tutacheza michezo ya kirafiki na timu za Coastal na African Sports kwa ajili ya kupima ubora wa kikosi chetu,” alisema Maganga.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.