Azam FC wamefikisha pointi 33 wakiwa katika uongozi wa ligi wakifuatiwa na Yanga wenye point 32 wakiwa wote wameshuka uwanjani mara 15.
Azam FC leo walikuwa katika uwanja wake waq Azam complexs uliopo Chamanzi kuwakaribisha wajeda wa Rhino Rangers na kuibuka na ushindi wa goli 1-0.
Tcheche akitafuta namna ya kumtoka mlinzi wa Rhino |
Goli hilo limemfanya mfungaji bora wa msimu uliopita Tcheche amfikie mshambuliaji wa Simba Hamisi Tabwe aliyefunga magoli 10 ambayo Tcheche ameyafikisha hi leo
Azam FC hii leo waliwakilishwa na Mwadini Ally, Maliki Ndeule, Erasto Nyoni, Aggrey Morrice, Said Moradi, Kipre Bolou, Himid Mao, Salum Aboubakari,Kone, Kipre Tcheche na Joseph Kimwaga
0 Maoni:
Post a Comment