Tuesday, March 11, 2014

MICHEZO ILIYOSALIA YA AZAM FC

Posted By: kj - 8:15 AM

Share

& Comment

http://azamfc.co.tz/sites/default/files/imagecache/pimage/publish/azam_6.jpg
Wakati baadhi ya timu zikieleka kucheza mchezo wao wa 22 wa ligi kuu ya vodacom, vinara wa ligi hiyo Azam FC wako katika mawindo ya kuwakabili Coastal Union ya Tanga katika mchezo wao wa 19 wa ligi kuu ya vodacom siku ya jumamosi machi 15 mwaka huu.

Azam FC kama ilivyokuwa katika misimu miwili iliyo pita mpaka kufikia michezo ya 19 walikuwa bado wamo katika mbio za Ubingwa na kwa mara ya pili mfululizo mbio za ubingwa zinabakia kwa Yanga na Azam FC.

Yanga jumamosi wao watakuwa wanacheza mchezo wao wa 18 wa ligi kuu ya vodacom dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Jamhuri kabla ya kuikabili Azam FC siku ya jumatano machi 19 mwaka huu.

Azam FC ambayo mpaka sasa haija poteza mchezo wowote ule ili wa twae ubingwa kwa mara ya kwanza inabidi kupata matokeo katika mechi 8 zilizo salia, amapo moja wapo ni dhidi ya Yanga iliyobakisha michezo 9 wakiwa na point 39 point moja nyuma ya Azam FC yenye pointi 40.

Kati ya michezo 8 iliyosalia kwa Azam FC michezo mitatu atakuwa katika uwanja wake wa Azam complex, miwili katika uwanja wa Taifa, michezo minmgine katika uwanja wa Sokoine, Mabatini na Mkwakwani.

Azam FC michezo aliyobakisha:

15/03/14  
AZAM FC Vs COASTAL UNION, U/azam

19/03/14
YANGA Vs AZAM FC, U/Taifa

26/03/14  
AZAM FC Vs SIMBA SC, U/Taifa

02/04/14  
RUVU SHOOTINGS Vs AZAM FC, Mabatini

06/04/14  
MGAMBO JKT    Vs AZAM FC, Mkwakwani

09/04/14  
AZAM FC Vs JKT OLJORO, U/Azam

23/04/14  
MBEYA CITY    Vs AZAM FC, Sokoine

27/04/14
JKT RUVU Vs AZAM FC, U/Azam

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.