Monday, August 3, 2015

MAANDALIZI YA NGAO YA JAMII KUANZA IJUMAA

Posted By: kj - 9:02 PM

Share

& Comment

Mara baada ya mchezo wa fainali wa kombe la kagame ambao ulimalizika kwa Azam FC kuibuka na ushindi wa goli 2-0, wachezaji wa Azam FC wamepewa mapumziko mpaka siku ya ijumaa.

Msemaji wa Azam FC Japhari Iddi Maganga amesem kuwa wachezaji wote wa Azam FC wamepewa mapumziko mpaka siku ya ijumaa, ambayo watarejea Chamanzi kwa ajili ya maandalizi na mchezo dhidi ya Yanga, agosti 22 mwaka huu.

Japhari Iddi Maganga amesema kuwa baada ya kurejea wachezaji watafanya mazoezi siku mbili kabla ya jumapili kuelekea Zanzibar kuweka kambi ya wiki mbili ya maandalizi ya mchezo huo wa ngao ya jamii.

Azam FC na Yanga wanataraji kukutana katika mchezo wa ngao ya jamii unao ashiria kuanza msimu mpya wa ligi kuu ya vodacom agust 22 mwaka huu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Wakati Azam FC wakitaraji kwenda Zanzibar, wapinzani wao teyari wapo Mbeya kwa ajili ya maandalizi ya mchezo huo.
a

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.