Friday, May 3, 2013

AZAM KUSHUKA UWANJANI SAA MOJA USIKU KWA SAA ZA BONGO KESHO

Posted By: azam fans - 11:20 PM

Share

& Comment

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) linaitakia kila lakheri timu ya Azam katika mechi yake ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika itakayochezwa Morocco kesho (Mei 4 mwaka huu).

Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano hiyo itachezwa jijini Rabat kuanzia
saa 11 jioni kwa saa za Morocco, ambapo ni sawa na saa 1 moja usiku kwa saa za Afrika Mashariki..

Timu hizo zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es salaam wiki mbili zilizopita.

Azam iko nchini Morocco kwa karibu wiki nzima sasa ikijiandaa kwa mechi hiyo chini ya Kocha wake Stewart John Hall. Msafara wa Azam nchini humo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF Eliud Mvella.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.