Saturday, August 24, 2013

AZAM FC WATOA SARE NA MTIBWA

Posted By: Unknown - 6:26 PM

Share

& Comment

Makamu bingwa wa ligi kuu ya vodacom Azam FC wameanza vibaya msimu mpya wa ligi kuu ya vodacom baada yak uwambulia sare ya goli 1-1 toka kwa wakatamiwa wa Turiani Mtibwa sugar mchezo uliochezwa katika uwanja wa Manungu Complex.

Katika mchezo huo ambao Mtibwa sugar waliutawala na kuipa kazi ya ziada ngome ya Azam FC walikuwa wa mwanzo kupata goli katika dakika ya 6 kupitia kwa mshambuliaji wao chipukizi Juma Lizao akiunga vyema pande la kiungo mchezeshaji wazamani wa SC Villa na Simba SC Shabani Kisiga.

Goli hilo liliendelea kuwapa nguvu Mtibwa sugar ya kulishambulia lango la Azam FC lakini jitihada ya mlinda mlango kinda Aishi Manula pamoja na safu yake ya ulinzi iliweza kuondosha hatari hizo.

Azam FC walisawazisha goli hilo kwa mkwaju wa penati uliopigwa na beki Aggrey Morice na kupelekea mchezo kwenda mapumziko milango ikisomeka 1-1.

Azam FC walianza kipindi cha pili kwa kufanya mabadiliko ambapo aliingi Kipre Bolue katika nafaci ya Himid Mao na Khamisi Mcha katika nafasi ya Ibrahim Mwaipopo mabadiliko ambayo yalipelekea timu hizo kushambuliani kwa zamu.

Katika dakika mbili za nyongeza kama Azam FC wangekuwa makini wangeweza kupata goli la ushindi baada ya kulisaka lango la Mtibwa Sugar kwa dakika zote mbili ikiwa Mtibwa Sugar wakitokea kupoteza nafasi kupitia kwa Mussa Mgosi, na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare ya goli 1-1

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.