Monday, August 26, 2013

AZAM FC WATUA SALAM TABORA

Posted By: Unknown - 6:53 AM

Share

& Comment


Na Mahmoud Zubeiry, Tabora BIN ZUBEIRY

KIKOSI cha Azam FC kimewasili usiku jana (jumapili agosti 25) mjini Tabora, kikitokea Morogoro tayari kwa mchezo wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumatano dhidi ya wenyeji, Rhino Rangers Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini hapa.

Azam imefika majira ya saa 4:30 tangu iondoke asubuhi mjini Morogoro na imefikia katika hoteli ya Mwafrika, jirani kabisa na Uwanja wa Mwinyi. 

Meneja wa Azam FC, Jemadari Said Kazumari amesema timu itapumzika kutwa ya kesho na jioni itafanya mazoezi, kujiandaa na mchezo huo unaosubiriwa kwa hamu na wakazi wa mjini hapa.
Wako Mboka Manyema; Wachezaji wa Azam kulia John Bocco, Erasto Nyoni katikati na kushoto Said Mourad

Azam ilianza Ligi Kuu kwa sare ya kufungana bao 1-1 na Mtibwa Sugar jana kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro.

Mtibwa walitangulia kupata bao kupitia kwa Juma Luizio dakika ya nne kabla ya Aggrey Morris kuisawazishia Azam kwa penalti dakika ya 19. 

Baada ya mechi hiyo, Azam inayofundishwa na kocha Muingereza, Stewart Hall ilikwenda kulala mjini Morogoro na asubuhi wakaondoka na basi lao kubwa la kisasa kuja Tabora, walipofika usiku huu.

Rhino, inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, nayo ilianza Ligi Kuu kwa sare ya kufungana 2-2 na Simba SC jana Mwinyi.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.