Sunday, February 2, 2014

AZAM WATOA DOZI NENE KWA KAGERA SUGAR

Posted By: Unknown - 7:36 PM

Share

& Comment

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjAoNquYhIQUjjYyY9UYqOibwKcuhyphenhyphen2FrjuOEtxre-87pZdiT41ncQQESkYVc3PulTuV4tUoxu1-2Oh1J1TXIiwRoQpAqb3vzxNezgubksuYXoFj91vWgeKpeL4NvuDQvOvkvc5uCBmZg8/s1600/2.JPG
Azam FC imeendeleza wimbi lake la ushindi katika michezo ya ligi kuu ya vodacom baada ya leo kuwa funga Kagera sugar goli 4-0 katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Azam complexs uliopo Chamanzi.

Katika mchezo huo Azam FC walianza kuandika goli la kwanza kupitia kwa mshambuliaji toka Uganda Brian Umonyi katika dakika ya 12 na kuipeleka Azam FC mapumziko wakiwa mbele kwa goli 1-0.

Katika kipindi cha kwanza chipukizi Joseph KImwaga alifanyiwa madhambi na kupelekea kutoendelea na mchezo.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiKiGu7O_5TGChZKjI4EMrM__uUt6eCwZoUSqZJmLEumpf7-SefdjOOM5U0kp1zw2sa6WNDHAVmB4W3OMgSLdfeTtmKdUbHTrAfyW8jCur-ic83grxer5kAIlN0k6-rivFHMNI2ox_zt44/s1600/1.JPG
Katika kipindi cha pili Azam FC walifanikiwa kuandika goli la pili kupitia kwa Brian Umonyi ikiwa ni dakika 3 baada ya kipindi hicho cha pili kuanza.

Dakika 3 mbele mshambuliaji chipukizi toka Azam Academy Kelvin Friday aliiandikia Azam FC goli la 3 na likiwa goli lake la kwanza katika kikosi cha Azam FC.

Kalamu ya magoli iliitimishwa na kiungo Jabir Azizi Stima katika dakika ya 83 na kuipelekea Azam FC kumaliza mchezo wakiwa na jumla ya goli 4-0, na kuendelea kuiweka kileleni Azam FC.
.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.