Wednesday, March 19, 2014

TCHECHE LAZIMA NI WAFUNGE YANGA

Posted By: kj - 2:55 PM

Share

& Comment

Mshambuliaji nyota wa Azam FC, Kipre Tchetche, raia wa Ivory Coast, ametuma salamu kwa wachezaji wa Yanga kwa kuwaambia kuwa watapata kazi ngumu ya kumzuia leo.

Yanga inavaana na Azam kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Timu hizo zilipokutana kwenye mzunguko wa kwanza, Azam iliibuka na ushindi wa mabao 3-2, hivyo mchezo huu unaonekana kuwa mkali kwa pande zote.

Kipre amesema anajua wazi kuwa mchezo huo utakuwa mkali lakini yeye na wachezaji wenzake watahakikisha wanatoka na pointi zote tatu ili kuzidi kujiimarisha kileleni mwa Ligi Kuu Bara.

Alisema hawaidharau Yanga lakini kwa kuwa yeye yupo Azam kwa ajili ya kuhakikisha wanafanya vizuri, basi ni wazi kuwa japo atapata upinzani mkubwa kutoka kwa mabeki wa Yanga, lazima ashinde kwa kuwa hiyo ndiyo kazi yake iliyompeleka katika timu hiyo.

 “Najua Yanga ni timu nzuri, itatupa upinzani mkubwa, lakini mimi nimekuja hapa Azam kwa ajili ya kufunga mabao na kuhakikisha timu inapata ushindi katika kila mechi, basi pia nitafanya hivyo katika mchezo na Yanga,” alisema Tchetche. 


CHANZO: SALEHE JEMBE

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.