Monday, January 26, 2015

AZAM FC KUWAFUATA TP MAZEMBE KESHO

Posted By: Unknown - 4:02 PM

Share

& Comment

Mabingwa wa ligi kuu ya Tanzania bara Azam fc wanataraji kuondoka kesho kuelekea DR Congo kwa ajili ya michuano mifupi iliyoandaliwa na TP Mazembe ya nchini humo, ambapo itachukuwa wiki moja.

Katika michuano hiyo inayoshirikisha timu nne ambazo ni TP Mazembe, Don Bosco ZESCO sambamba na Azam FC inataraji kuanza siku ya jumatano januari 29 mwaka huu.

Michuano hiyo inacheza kwa kuzikutanisha timu zote nne kwa hivyo kutoa furasa kwa kila timu kucheza michezo mitatu.

Azam FC inataraji kurejea nchini february 4 mwaka huu, na katika msafara huo utakao enda DR Congo utajumuisha wachezaji 24 ambao ni makipa Mwadini Ally, Aishi Salum, Jackson Wandwi na Khalid Mahadhi.

Mabeki ni Salum Kapombe, Agrey Morice, Pascal Wawa, Erasto Nyoni, David Mwantika, Said Morad na ardiel Michael.

Viungo ni Salum Aboubakri, Mudathir Yahya, Franky Domayo, Himid Mao, Amri Kiemba, Kipre Bolue na Khamis Mcha.

Washambuliaji ni Kelvin Firday, John Bocco, Brian Majegwa, Gaudency Mwaikimba, Dider Kavumbagu na Kipre cheche.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.