Sunday, July 12, 2015

ZUNGU AIFUNGIA AZAM FC GOLI LA KWANZA, IKIICHAPA COASTAL GOLI 1-0

Posted By: kj - 9:30 PM

Share

& Comment

Mshambuliaji mpya wa Azam FC toka visiwani Zanzibar Ame Ally 'Zungu' leo amefanikiwa kuifungia Azam FC goli lake la kwanza katika mchezo wake wa kwanza kuitumikia Aza mFC katika ushindi wa goli 1-0 mbele ya Coastal union.

Azam FC walicheza na Coastal union leo katika uwanja wa CCM Mkwakwani ukiwa mchezo wa kujiandaa na michuano ya Kombe la Kagaem.

Katika mchezo huo wa kirafiki, Ame Ally aliyesajiliwa akitokea Mtibwa Sugar alianzia benchi na alipoingia akaifungia Azam FC goli pekee katika mchezo huo na Azam FC kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

Azam FC wanataraji kurejea jijini Dar es salaam hii leo baada ya ziara ya siku 3 katika mji wa Tanga ambapo wamecheza micezo miwili ya kirafiki na kila mchezo kuibuka na ushindi wa goli 1-0.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.