Wednesday, February 6, 2013

SAMIH KUWAKOSA WASUDAN

Posted By: azam fans - 9:35 PM

Share

& Comment

Beki wa kushoto wa azam fa Samih Hajji Nuhu atakosa mchezo wa kombe la shirikisho (CAF confederation cup) kati ya Azam fc na Al-Nasri Juba ya Sudan kusini kufuatia kuumia kwa uti wa mgongo.

Samih alipata jeraha hilo la mgongo katika mchezo wa kirafiki kati ya azam na simba uliochezwa jumatatu asubuhi katika uwanja wa azam uliopo Chamanzi na azam kuibuka na ushindi wa goli 3-1.

Samih atakuwa nnje ya uwanja kwa kipindi cha mwezi mmoja na ataanza kwa kukosa mchezo wa ligi kuu ya vodacom dhidi ya mtibwa sugar utakao fanyika katika uwanja wa Manungu complex.

Samih aliyerejea katika uwanja msimu huu baada ya kuwa majeruhi kwa msimu mzima msimu uliopita wa 2011/12 baada ya kuumia katika duru la pili msimu wa 2010/11 na katika msimu huu alirejea kwa kasi na kurejesha namba yake iliyokuwa inashikiliwa na Waziri Salum akisaidiana na kiraka Erasto Nyoni.

--
MSUNI COMPUTER SOLUTION NDIO SULUHISHO LA TATIZO YA COMPUTER YAKO
www.aboodmsuni21.blogspot.com
[+255 657 184 421]

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.