Friday, September 27, 2013

KALLY: TUKO TEYARI KUVUNA POINTI 3 KWA PRINSONS

Posted By: azam fans - 2:55 PM

Share

& Comment

KALI WAKATI AKIICHEZEA AZAM...
Kocha Msaidizi wa Azam FC, Kally Ongala amesema wamejiandaa vya kutosha kwa ajili ya kukabiliana na wapinzani wao Tanzania Prisons.

Azam wanatarajiwa kuvaana na Prisons keshokutwa Jumapili katika mechi ya Ligi Kuu Bara mechi itakayochezwa kwenye Uwanja Sokoine Mkoani Mbeya.
Kocha huyo alisema kuwa kikosi kipo fiti kwa ajili ya mechi hiyo, hivyo mashabiki watarajie kupata matokeo mazuri.

“Wachezaji wote wana afya njema na wapo tayari kwa ajili ya kukabiliana na wapinzani wetu, hivyo mashabiki watarajie kupata matokeo mazuri kutokana na maandalizi tuliyofanya,” alisema Ongala. 

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.