Tuesday, November 26, 2013

ACADEMY WATINGA NUSU KUWAKABILI COASTAL

Posted By: Unknown - 10:48 PM

Share

& Comment

Mabingwa watetezi wa kombe la Uhai Azam academy leo wamefanikiwa kutinga hatua ya nusu baada ya kuwalaza goli 2-1 timu ya vijana ya Tanzania Prisons mchezo uliochezwa katika uwanja wa Azam complex.

Azam academy katika mchezo wa nusu fainali utakaochezwa siku ya Alhamisi kwenye uwanja wa Azam complexs na kuonyeshwa moja kwa moja na azam tv utakuwa dhidi ya coastal union.

Coastal union ambao waliwafunga AZam Academy katika mchezo wa makundi goli 2-1, wametimga hatua hiyo baada ya kuwalaza goli 1-0 timu ya JKTOljoro, mchezo uliochezwa mapema ya leo.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.