Monday, October 8, 2012

MSERBIA KUWANOA MAKIPA WA AZAM

Posted By: azam fans - 11:43 PM

Share

& Comment

Na Mahmoud Zubeiry

AZAM FC, washindi waMedali tatu za Fedha, Ligi Kuu msimu uliopita, Kombe la Urafiki na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, wameimarisha benchi lao la ufundi kwa kuleta kocha mpya kutoka Serbia, Slobodan.

Slobodan ametua Azam kwa kazi moja tu maalum, kuwanoa makipa wa timu hiyo inayo fukuzana na Simba kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Slobodan ni chaguo la kocha wa sasa wa Azam, kutoka Serbia pia, Boris Bunjak 'Boca' ambaye amerithi mikoba ya Muingereza Stewart Hall aliyefukuzwa Julai mwaka huu.


Source: BIN ZUBEIRY

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.