Friday, May 16, 2014

ABDALLAH KHERI ATUA AZAM FC

Posted By: Unknown - 5:58 AM

Share

& Comment

Klabu ya Azam FC imemsajili kwa mkataba wa miaka mitatu beki chipukizi wa kati, Abdallah Kheri Salum wa klabu ya Zimamoto ya Zanzibar.

Beki huyo mwenye uwezo pia wa kucheza nafasi ya kiungo, kwa sasa yupo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes.

Katibu mkuu wa Azam FC, Nasoro Idrisa, alisema: “Ni mchezaji mdogo mwenye kipaji, ambaye wasaka vipaji wetu wamejiridhisha kuwa atakuwa msaada kwa timu yetu baadaye. Hivyo tumeamua kumpa mkataba wa miaka mitatu.”

Naye Salum alisema amefurahia kujiunga na ‘Wana lambalamba’ hao kwa vile ni miongoni mwa timu kubwa na aliahidi kutumia fursa hiyo kuendeleza kipaji chake.

“Azam ndiyo mabingwa wa Tanzania Bara. Ni timu kubwa na bora ambayo naamini ni bahati kwangu kujiunga nayo. Ninaamini nitaendeleza kipaji changu na kutimiza ndoto za kuwa mchezaji bora baadaye,” alisema Salum.

Kinda huyo anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Azam baada ya kumalizika kwa msimu huu na kutwaa taji la kwanza la ubingwa wa Tanzania Bara.

Wengine walionaswa na Azam ni kiungo Frank Domayo na mshambuliaji Didier Kavumbangu waliojiunga na timu hiyo wakitokea Yanga, pamoja na mshambuliaji Ismaila Diara kutoka Mali.

Mkakati mwingine wa klabu hiyo ni kumsajili kiraka, Shomari Kapombe kutoka AS Cannes ya Ufaransa.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.