Azam FC ambayo ipo DR Congo wameobwa na FC Lupopo kucheza mchezo wa kirafiki baada ya michuano maalum ya TP Mazembe yaliyoanza jana kumalizika.
“Nadhani Lupopo wamevutiwa na sisi, wameomba tucheze nao lakini bado hatujaamua itakuwa lini,” alisema Meneja wa Azam FC Jemedari Saidi.
Azam FC jana imecheza mchezo wake wa kwanza kati ya mitatu itakayo cheza katika mashindano hayo mafupi yaliyo andaliwa na TP Mazembe, ambao Azam FC walikubali kufungwa goli 1-0 dhidi ya wenyeji wao TP Mazembe.
0 Maoni:
Post a Comment