Moradi aliyejiunga na Azam FC akitokea Kagera sugar mkataba wake ulimalizika mwezi machi sambamba na beki Erasto Nyoni.
Msemaji wa Azam FC Japhari Iddi amesema kuwa Azam FC imewaongezea mkataba wachezaji wake watatu ambao mikataba yao imekuwa imekwisha ambao ni Said Moradi, Erasto Nyoni na Didier Kavumbagu.
Japhari alisema kuwa kumalizika kwa mikataba ya Erasto na Morad kulisababisha kukosekana kwao katika michezo ya mwisho ya ligi.
Morad amekuwa akihusishwa na kurejea Simba SC kabla ya kusaini mkataba, mpya wa kuitumikia Azam.
Morad alipata kupitia Simba kabla ya kujiunga na Kagera sugar, ambapo Simba walimchukuwa kutoka Ashanti united ya Ilala jijini Dar es salaam.
0 Maoni:
Post a Comment