Migi alitua nchini siku ya jumatano na kujiunga na Azam FC moja kwa moja katika mazoezi ya Azam FC na kufanikiwa kucheza michezo miwili ya Kirafiki dhidi ya Coastal Union na African Sport ambapo Azam FC walishinda kwa goli 1-0 katika michezo yote waliyo cheza.
Migi anakuwa mchezaji wa 6 wakigeni katika kikosi cha Azam FC na kufanya ibakie nafasi moja ambayo itakuwa inawaniwa na wachezaji wanne waliopo Chamanzi kwa ajili ya majaribio, ambapo nafasi kubwa ya kujaza nafasi hiyo anapewa Muingereza Ryan Burge.
Migi anatajiunga na timu yake ya APR katika michuano ya kombe la Kagame kabla ya kurejea kuitumikia rasmi Azam FC baada ya michuano hiyo inayoanza jumamosi kumalizika.
Wachezaji wengine wanao saka nafasi hiyo moja ya kusajiliwa na Azam FC ni pamoja na Nelson Lukong kutoka Cameroon, Vincent Atchouailou de Paul Angban kutoka Ivory Coast na Allan Wetende Wanga kutoka Kenya.
0 Maoni:
Post a Comment