Wednesday, January 20, 2016

KAWEMBA AFANUNUA KILICHO WAKWAMISHA FARID NA KELVIN

Posted By: kj - 9:01 AM

Share

& Comment


DILI la wachezaji wa Azam FC, Kelvin Friday na Farid Mussa kucheza soka la kulipwa nje ya Tanzania limekuwa gumu.

Friday alifuzu kucheza katika klabu ya St. George ya Ethiopia baada ya kwenda kufanya majaribio ya wiki mbili hivi karibuni, wakati Mussa alikuwa anatakiwa na timu moja ya Slovenia iliyokuwa imeweka kambi Hispania.

Akizungumza na gazeti hili, Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba alisema kuwa Friday baada ya kufuzu, timu hiyo ya Ethiopia ilisema ingekuja kufanya mazungumzo lakini haifanya hivyo.

“St. George ilionesha nia kwa sababu mchezaji alishafuzu, lakini baadaye hawakuonekana tena, kwa hiyo mchezaji mwenyewe kwa sababu tulimpeleka Mtibwa kwa mkopo tukamwambia aendelee na timu hiyo,” alisema.

Aidha, kwa upande wa Mussa, Kawemba alisema wakati timu iko Zanzibar walikuwa wakimhangaikia mchezaji na alikuwa tayari amepata hati ya kusafiri, lakini kilichotokea kuna baadhi ya vitu walitakiwa kuwa navyo.

“Mambo yalikuwa yanaenda vizuri, tulipata hati ya safari kule ubalozini lakini kuna vitu walihitaji tuwape na kwa wakati huo hatukuwa navyo, kwa hiyo nikamwambia mchezaji aende Zanzibar kujiunga na wenzake na baadaye tutaendelea,” alisema.

Kawemba alisema kwa vile Mussa bado umri wake ni mdogo wataendelea kumuimarisha kiwango chake kwa kuwa bado kuna timu za Ulaya zimeonesha nia ya kumhitaji na mambo yakiwa sawa wataweka wazi.

Chanzo: Habari leo

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.