Tuesday, January 26, 2016

KITAMBI: AZUNGUMZIA USHINDI WA AZAM MBELE YA LYON

Posted By: kj - 9:18 AM

Share

& Comment


Akizungumza na mtandao wa www.azamfc.co.tz mara baada ya mchezo huo, Kocha Msaidizi wa Azam FC, Dennis Kitambi, alisema kuwa wamefurahishwa na ushindi mnono walioupata huku akidai kuwa wanakabiliwa na mtihani mgumu zaidi kwenye hatua waliyovuka.

“Mechi haikuwa rahisi, tunamshukuru Mungu kwa kupata ushindi mnono wa mabao manne, katika hatua ijayo tunaweza kupata timu ambayo ni ya Ligi Kuu, hivyo tutahakikisha tunajipanga vema na kuhakikisha tunazidi kufanya vizuri,” alisema.


Katika hatua nyingine alidai kuwa wamefurahishwa na kiwango alichoonyesha Migi kwenye majukumu mapya ya kucheza beki ya kati akichukua mikoba ya Pascal Wawa.

“Tumefurahishwa na kiwango alichoonyesha Migi, amecheza vizuri kama beki wa kati na tuliona anaweza kufanya hivyo mara baada ya kuumia kwa Wawa (Pascal),” alisema.

Azam FC mara baada ya mchezo huo, usiku wa kuamkia leo iliondoka nchini kwa usafiri wa ndege kuelekea jijini Ndola, Zambia kwa ajili ya kushiriki michuano maalum iliyoandaliwa kwa ushirikiano na wenyeji wao, Zesco United na Zanaco.

Mbali na timu hizo tatu zitakazoshiriki michuano hiyo itakayoanza kesho Jumatano hadi Februari 3 mwaka huu, nyingine ni mabingwa wa Zimbabwe Chicken Inn, ambao wataanza kufungua dimba dhidi ya Zanaco siku hiyo saa 8.00 mchana kwa saa za hapa huku Azam FC ikikipiga na Zesco United saa 10.00 jioni.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.