Tuesday, July 19, 2016

AZAM KUWAKABILI FRIENDS RANGERS KESHO ASUBUHI

Posted By: kj - 5:01 PM

Share

& Comment

Wakati Azam FC ikiendelea na programu yake ya maandalizi ya msimu ujao kwa siku ya 12 leo, kesho Jumatano inatarajia kucheza mechi ya pili ya kirafiki dhidi ya Friends Rangers inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL) itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex saa 3.00 asubuhi.

Jumapili iliyopita Kocha Mkuu wa Azam FC, Zeben Hernandez, aliiongoza timu hiyo kwenye mchezo wake wa kwanza na kwa kuifunga Ashanti United mabao 2-0.

Katika mazoezi hayo ya leo, Azam FC ilimpokea kwenye majaribio mshambuliaji raia wa Burundi, Fuadi Ndayisenga, aliyetokea Sofapaka ya Kenya alipofunga mabao nane msimu uliopita.

Ndayisenga anaungana na wachezaji wengine watatu waliokuwa kwenye majaribio, beki wa timu ya Taifa ya Niger, Mohamed Chicoto na mshambuliaji kutoka huko Mossi Moussa Issa pamoja na Ibrahima Fofana wa Ivory Coast.

Azam FC itacheza mchezo mwingine wa kirafiki Jumamosi ijayo dhidi ya Halmashauri ya Kinondoni (KMC) kabla ya Jumatatu ijayo kutimkia Zanzibar kwa ajili ya kambi ya kutafuta utulivu kwa wachezaji wakati wakipokea mazoezi ya kiufundi kabla ya kurejea na kufanya maandalizi ya mwisho kabla ya kuvaana na Yanga kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii Agosti 17, mwaka huu.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.