Wednesday, January 25, 2012

Azam wafungua duru la pili kwa ushindi

Posted By: kj - 7:33 PM

Share

& Comment


Mabingwa wa mapinduzi Cup wameanza salama safari ya duru la pili la kusaka ubingwa wa Tanzania Bara, baada ya kuwachapa goli 2-1 African lyon.

Azam FC walianza safari yao kwa goli la kujifunga Lyon na baadae kidogo Lyon kusawazisha goli hilo kupitia kwa Semi Kessi.

Azam ambao wanasifika kwa pasi nyingi walipata goli la pili kupitia kwa Mfungaji bora wa wakati wote wa Azam John Bocco Adbayor aliyefunga goli lake la 8 msimu huu.

Azam FC watarejea uwanjani tena jumapili january 29 dhidi ya Moro united, na sasa wako katika nafasi ya 3 wakiwa na point 26 nyuma kwa point 2 kwa Yanga na point 5 kwa kinara Simba SC.

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © 2025 CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.