Wednesday, January 4, 2012
Mwaikimba aiokoa Azam FC
Posted By: kj - 7:47 PMMshambuliaji mpya wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba ameipatia point moja timu ya Azam FC pale walipo wakabili Mafunzo FC walio wafunza Soka Yanga.
Katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja Amani, Mafunzo FC walikuwa wa mwanzo kupata goli katika dakika ya 12 kabla ya Mwaikimba kuisawazishia Azam FC.
Katika mchezo huo ulishuhudia urejeo wa Mrisho Khalfan Ngassa katika kikosi kufuatia jeraha alilolipata pale Azam FC walipocheza na Yanga mwaka jana katika mchezo wa kirafiki.
Azam FC inayoongoza Kundi B kwa kuwa na point 4 watawavaa Yanga siku ya ijumaa, katika mchezo wa mwisho wa makundi katika michuano hiyo ya mapinduzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Maoni:
Post a Comment