Wednesday, December 18, 2013

AZAM KUFUNGUA NA KOMBAINI YA UNGUJA MAPINDUZI CUP

Posted By: Unknown - 6:48 AM

Share

& Comment

Mabingwa watetezi wa kombe la Mapinduzi Azam FC na mabingwa wa Tanzania bara Yanga wamewekwa kwenye kundi moja katika michuano ya kombe la mapinduzi linalo tarajia kuanza januari 1 mpaka januari 13 mwakani.

Azam na Yanga wamewekwa kwenye kundi C samabamba na Tusker ya Kenya na Kombaini ya Unguja, huku Simba SC wakiwa katika kundi B pamoja na AFC Leopards ya Kenya, KMKM na KCC ya Uganda. Wakati kundi A linaundwa na timu za Mbeya City, kombaini ya Pemba, Chuoni na URA ya Uganda.

Simba SC watafungua na AFC Leopads siku ya january mosi kuanzia saa 2 usiku, huku Januari 2 kukiwa na michezo minne katika viwanja vya Amani Unguja na uwanja wa Gombani Pemba.

Katika uwanja wa Amaan, Azam FC wataonyeshana kazi na Unguja Combine kuanzi saa 10:00 alasiri ukifuatiwa na mchezo kati ya Yanga na Tusker itakayorindima kuanzia saa 2:00 usiku.

Na katika uweanja wa Gombani shughuli itakuwa kati ya URA na Chuoni (kundi A) watakaovaana saa 8:00 mchana, huku Mbeya City ikitoana jasho na Pemba Combine, saa 10:00 jioni katika mchezo wa kundi A.


KUNDI A:
URA (Uganda)
Chuoni
Mbeya CityPemba Combine

KUNDI B:
SImba SC
AFC Leopard (Kenya)
KMKM
KCC (Uganda)

KUNDI C:
Yanga SC
Azam FC
Tusker (Kenya)
Kombaini ya Unguja



0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.