Tuesday, September 9, 2014

AZAM KAMILI KUIVAA YANGA JUMAPILI

Posted By: Unknown - 5:17 AM

Share

& Comment

https://m.ak.fbcdn.net/photos-a.ak/hphotos-ak-xaf1/v/t1.0-0/p320x320/10600389_818374448202913_2167620276583148869_n.jpg?oh=0f24c89d850401f7a8ed304f1d283603&oe=5488D0A6&__gda__=1419688513_3bdb0d8c58ea61daae12ab46630d410b
MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Azam FC wameendelea na maandalizi yake kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga utakaochezwa Jumapili wiki hii kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog alisema kikosi chake kipo tayari kwa ajili ya mchezo huo wa Jumapili na faraja kubwa kwake ni kurudi dimbani kwa beki wake kisiki, Aggrey Moris aliyekuwa akisumbuliwa na malaria yalisababisha ashindwe kusafiri na timu ya taifa ‘Taifa Stars’.



“Kwa ujumla tumeshamaliza maandalizi na kikosi changu kipo tayari kwa ajili ya mchezo na Yanga pamoja na Ligi Kuu kwa sasa sina majeruhi baada ya Moris kuanza mazoezi leo (jana) na Jumatano, Didier Kavumbagu atakuwa amerudi kutoka kumaliza majukumu yake ya timu yake ya taifa,” alisema Omog.

Ukiacha kurejea uwanjani kwa nyota hao, Omog alisema anafurahi kuona mshambuliaji raia wa Haiti, Lionel Saint Preux anaendelea vizuri na mazoezi baada ya kuumia goti wakati akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo Azam Complex.
 
 

https://m.ak.fbcdn.net/photos-c.ak/hphotos-ak-xap1/v/t1.0-0/q84/s320x320/10641227_819539264753098_7787275441950861920_n.jpg?oh=0d7dbd76bfb2e9606811b57b0f15c3e4&oe=549E1080&__gda__=1419469841_cb31e9a34197e17676da816978b7519a
Beki kisiki Agrey Morice
“Preux anaendelea vizuri na mazoezi tangu wiki iliyopita baada ya kupona maumivu ya goti na atakuwepo kwenye mchezo wa Jumapili najua mchezo utakuwa mgumu, lakini lengo letu ni kuhakikisha tunashinda ili kujiwekea mazingira mazuri ya kuanza ligi vizuri,” alisema kocha huyo raia wa Cameroon.

Hiyo ni mara ya pili kwa timu hizo kucheza mechi ya Ngao ya Jamii ambapo msimu uliopita timu hizo zilikutana na Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa katika dakika ya pili na kiungo Salum Telela.


chanzo: habari keo

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.