![]() |
Kiemba akiwa zoezini na uzi wa azam fc |
Lakini akaenda mbali na kuwaambia mabosi wake wa sasa, yeye hajui kuchagua, wampe jezi yenye namba yoyote ile iliyopo au watakayoona inamfaa ataivaa.
Kiemba amekwenda Azam kwa mkopo na dau la Sh10 milioni akitokea Simba.
Mchezaji huyo ameliambia Mwanaspoti kuwa: “Tukijaaliwa kesho (leo) nitaanza mazoezi rasmi. Binafsi nimejiandaa vizuri lakini siwezi kutoa ahadi nyingi kila kitu nimemwachia Mungu aamue.”
“Unajua wakati mwingine binadamu tunakosea, unasema nitafanya hiki na hiki lakini utambue kuwa yote yanapangwa na Mungu kikubwa naomba ushirikiano,”alisema Kiemba ambaye amebakiza miezi sita Simba na amekwenda kwa mkopo Azam kwa miezi sita.
“Unaweza kukuta, hata hicho kilichonitokea Simba, ilipangwa tu ili kifanyike hiki kilichofanyika.”
Akizungumzia sakata lake Simba, Kiemba alisema:
Hadi kutua kikosini hapo, Kiemba alikuwa amesimamishwa na uongozi wa Simba kwa kile kinachodaiwa ni utovu wa nidhamu. Alisimamishwa pamoja na wachezaji wenzake, Shaaban Kisiga ‘Marlone’ na Haroun Chanongo.
0 Maoni:
Post a Comment