Mchezo wa ligi kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam FC na Simba SC na ule wa Azam FC na Yanga SC iliyokuwa ichezwe katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, sasa kuchezwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mabadiliko hayo yalisababishwa na kufungwa kwa Uwanja wa Taifa pamoja na Azam Stadium kuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki wachache. Na uwanja wa Uhuru uliokuwa unatumiwa na Azam kama uwanja wake wa nyumbani pia umefungwa.
Mechi ya Azam na Simba utakao chezwa september 10, ambapo Azam atakuwa mwenyeji umepangwa kufanyika katika uwanja wa Mkwakwani huko Tanga.
Wakati ule wa yanga ambapo Azam atakuwa mwenyeji unatazamiwa kupigwa katika uwanja huo wa Mkwakwani.
Tuesday, September 6, 2011
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

SIB 90
POPULAR
TAGS
0 Maoni:
Post a Comment