Azam fc siku ya jumatano ya marchi 27 watakuw wenyeji wa Prinsons katika uwanja wa Azam Complexs uliopo Mbande jijini Dar es salaam, mchezo ambao azam fc watacheza bila ya kocha Stewart Hall ambaye anatumikia adhabu ya kukosa michezo mitatu.
Hall alifungiwa na TFF michezo mitatu na huo wa jumatano dhidi ya Prisons utakuwa wa pili na adhabu yake kufikia kikomo mwisho mwajuma hili pale azam watakapo wakabili Ruvu Shooting.
Akizungumzia kambi yake iliyoanza leo kocha Stewart Hall amesema kuwa safari hii hana majeruhi yoyote ule baada ya beki Samir Hajji Nuhu kupona jeraha lake lililo muweka nnje ya uwanja kwa takribani wiki nne sasa.
Kambi hiyo ya azam fc itawekwa katika hosteli za timu hiyo zilizopo ndani ya azam complex nnje ya jiji la Dar es salaam Mbande.
--
MSUNI COMPUTER SOLUTION (Tunarejesha uhai wa computer)
www.aboodmsuni21.blogspot.com/p/msuni-computer-solution_7934.html
0 Maoni:
Post a Comment