Tuesday, March 26, 2013

HUMUDI KUELEKEA BONDENI

Posted By: kj - 5:42 PM

Share

& Comment

Kiungo wazamani wa Ashanti United, Mtibwa sugar na Simba SC Abdulhalim Homoud anatarajia mwishoni mwajuma kwenda Afrika kusini 'Bondeni' kwa ajili ya majaribio katika timu ya Jomo Cosmos ya nchini humo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowekwa katika tofuti ya azam fc inayommiliki mchezaji huyo kwa sasa zinaeleza kuwa Humuod amepata nafasi hiyo katika timu hiyo (Cosmos) inayopambana kurejea ligi kuu ya Afrika kusini (PSL) baada ya viongozi wa azam fc kumfanyia mpango, ikiwa ni katika utimizaji wa agenda ya kutengeneza uwanja mpana kwa wachezaji wa Tanzania kupata nafasi katika ligi mbalhmbali.

Cosmos ina milikiwa na aliyewahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Afrika kusini (Bafana bafana) Jomo Somo. Vilevile ishawahi kutumikiwa na watanzania Nteze John na Ally Shah.
--
MSUNI COMPUTER SOLUTION (Tunarejesha uhai wa computer)
www.aboodmsuni21.blogspot.com/p/msuni-computer-solution_7934.html

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.