Katika msafara huo utawajumuisha wachezaji wote waliosajiliwa kwa ajili ya michuano hiyo ukiwaondoa Samih Hajji Nuhu aliyemajeruhi na kiungo Abdulhalim Homoud aliyejiunga na Cosmos ya Afrika kusini.
Vile vile benchi lote la ufundi linaloongozwa na Muingeleza Stewart Hall utakuwa miongoni mwa sehemu ya msafara huo.
Hata hivyo uongozi wa azam fc teyari wameshatanguliza watu nchini Moroco kwa ajili ya kuweka mazingira sawa yatakayo fikiwa na kikosi chao.
Azam fc katika mchezo huo utakao chezwa mei 5 mwaka huu wanatakiwa kutoka na ushindi ama sare ya magoli kufuatia mchezo wa awali kwisha kwa sare ya bila kufungana.
0 Maoni:
Post a Comment