Saturday, December 7, 2013

AZAM COMPLEX KUTUMIA TIKETI ZA ELKTRONIA MWAKANI

Posted By: Unknown - 6:13 AM

Share

& Comment

MATUMIZI ya tiketi za kisasa za kieletroniki katika viwanja vitakavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara, yataanza kwa majaribio katika Uwanja wa Azam Complex kuanzia mwakani.

Awali, mfumo huo unaolenga kudhibiti mapato na kuondoa usumbufu kwa mashabiki kupanga foleni siku za mechi, ulipangwa kuanza mwaka jana na baadaye kuahirishwa na kutakiwa kuanza Januari, lakini imeshindikana kutokana na kudaiwa kukawia kuwasili kwa mashine zitakazofungwa katika viwanja husika.

Akijibu maswali ya waandishi wa habari Dar es Salaam wiki hii, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Jamal Malinzi alisema tayari mashine zimeshafungwa karibu viwanja vyote isipokuwa viwili kile cha Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora na cha Kaitaba mjini Bukoba mkoani Kagera.

“Kudhibiti wizi wa tiketi ni changamoto kubwa, lakini niseme kwamba suala hilo tutalifanyia kazi, lakini kwa kuanza majaribio kwenye Uwanja wa Azam Complex, ndipo tutaendelea na sehemu nyingine,” alisema Malinzi aliyeingia madarakani Oktoba 27, mwaka huu.

Alisema lengo la kuanza na uwanja mmoja ni kutaka kuona kwanza utendaji wake utakavyokuwa, kama utasaidia ndipo viwanja vingine vitaruhusiwa kuendelea na mpango huo.

Mpango wa kutumia mfumo huo ni matokeo ya juhudi mbalimbali za TFF kutafuta njia bora itakayodhibiti mapato ya viwanjani na kuondoa usumbufu kwa wapenzi kupanga foleni siku ya mechi au siku chache kabla.

Kufanikiwa kwa mfumo huo ni baada ya Benki ya CRDB, kushinda zabuni ya kazi hiyo baada ya mchakato ulioshirikisha kampuni mbalimbali zilizotuma maombi yao.


CHANZO: HABARI LEO

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.