Saturday, March 22, 2014

UMONYI, AGGREY KUREJEA KESHO UWANJANI

Posted By: kj - 5:06 PM

Share

& Comment

Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam

MSHAMBULIAJI Mganda, Brian Umony anatarajiwa kurejea uwanjani kesho timu yake, Azam FC ikimenyana na JKT Oljoro katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Umony alitarajiwa kurejea uwanjani katikati ya wiki Azam ikimenyana na mabingwa watetezi, Yanga SC na kutoka sare ya 1-1 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, lakini alijitonesha siku mbili kabla ya mchezo huo. 
Rasta anarudi;Brian Umony anatarajiwa kurejea uwanjani kesho baada ya kukosa mechi mbili
Aggrey Morris pia anatarajiwa katika mchezo wa kesho na JKT Oljoro

Umony amekosa mechi mbili mfululizo zilizopita za Azam FC kutokana na maumivu ya kifundo cha mguu, lakini kesho kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog anaweza kumuanzisha.

Beki Aggrey Morris aliyeshitua nyama katika mchezo na Coastal Union Chamazi, Azam FC ikishinda 4-0 hata akakosa mechi iliyopita na Yanga, naye kesho anatarajiwa kurejea uwanjani dhidi ya Oljoro.

Azam FC ambayo itamkosa beki wake wa kulia Erasto Nyoni anayetumikia adhabu ya kadi mbili za njano alizopewa katika mechi moja na Yanga, itamkosa pia na beki Sammih Hajji Nuhu ambaye bado majeruhi sawa na viungo Ibrahim Mwaipopo, Farid Mussa na Joseph Kimwaga.

Azam FC kesho itajaribu kujivuta mbele zaidi kileleni mwa ligi hiyo katika mbio za ubingwa itakapomenyana na Oljoro ikihitaji kujiongezea pointi kutoka 44 ilizonazo sasa baada ya mechi 20.


KUTOKA KWA: BIN ZUBEIRY

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.