Tuesday, July 15, 2014

WAWILI KUFUNGA USAJILI WA AZAM FC

Posted By: Unknown - 6:53 PM

Share

& Comment

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic1ex46YneZTPousxp9xSPJePLWRVDsksFqn0HA-XxW5lIHvSDGpauPQNGGD0fvgsEJes8GeuF0dkroTIo-9HwJWXPDbAy5DLAbvtt-JdtVdAyPvYp8dZn5DMJ8nWGlKrTOyE8YqsfGac/s640/1397179_669015719805454_1383073960_o.jpg


KLABU ya Azam FC kwa sasa imeingia vitani kusaka wachezaji wawili kuongeza nguvu katika nafasi ya winga pamoja na kiungo.

Awali klabu hiyo ilitaka kumsajili kiungo wa zamani wa Yanga, Athumani Idd ‘Chuji’ lakini waliamua kuachana na mpango huo kutokana na rekodi mbaya ya nidhamu ya mchezaji huyo.

Azam imepania kupata kiungo huyo kwa sasa hasa baada ya kuumia kwa kiungo wao mpya Frank Domayo aliyefanyiwa operesheni ya nyama za paja na atakaa nje ya uwanja kwa miezi tisa.

Wakizungumza na Mwanaspoti, Kocha mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog na meneja wa timu hiyo, Jemedari Said wamesema tayari uongozi wa klabu hiyo umebariki mpango huo, hivyo kwa sasa wanaangalia wachezaji wanaokidhi mahitaji yao kwa sasa.

“Tumependekeza kwa uongozi kuongezewa nguvu ya wachezaji wawili, mmoja atakuwa ni kiungo na mwingine ni winga, hilo linabidi kufanyika katika majira haya ya usajili na mpaka sasa wapo baadhi ya wachezaji tunaowahitaji,” alisema Omog.

Meneja wa timu hiyo, Jemedari alisema kuwa “Muda wa usajili bado upo hivyo tutafanya kwa umakini zaidi ili kuwapata wachezaji hao watakaotufaa,”.

Wakati huohuo, Omog alisema kuwa kuanzia wiki hii kikosi chake kitaanza kucheza mechi za kirafiki mara mbili kwa wiki ambapo leo Jumanne asubuhi Azam watacheza na Polisi Moro iliyopanda daraja, mechi hiyo itachezwa Chamazi.

“Wachezaji wanaendelea vizuri, wameonyesha ukomavu mzuri kwa sasa tumepanga kuwa na mechi mbili za kirafiki kila wiki ili tuweze kuona sehemu zenye upungufu na kuziboresha zaidi.” alisema Omog.


CHANZO: MWANASPOTI

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.