Wednesday, August 27, 2014

AZAM FC KUANZA MAZOEZI KESHO

Posted By: Unknown - 10:33 PM

Share

& Comment

MABINGWA wa Bara, Azam FC wanatarajiwa kuanza tena mazoezi kesho Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam baada ya kurejea kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda.
 
Katibu wa Azam FC, Nassor Idrissa Mohammed ‘Father’ ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba wachezaji wote wataanza mazoezi kesho, kasoro wale ambao wameitwa timu ya taifa.

Father amesema kwamba wachezaji wawili, Aishi Manula na Kevin Friday japokuwa hawapo kwenye kikosi cha Taifa Stars, wao wamepewa mapumziko zaidi- hivyo si lazima waanze kesho.
Azam FC wanatarajiwa kuanza mazoezi kesho kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC Septemba 13, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

 
Aidha, Father alisema kwamba Simba SC waliomba mchezo wa kirafiki na wao wikiendi hii, lakini imeshindikana kwa sababu kocha Joseph Marius Omog amesema hawezi kuwa na mechi baada ya mazoezi ya siku mbili.
 
“Mwalimu amesema mchezo wanaotaka Simba SC labda wiki ijayo, kwa sababu hawezi kufanya mazoezi Alhamsi na Ijumaa halafu baada ya hapo awe na mechi, ngumu,”amesema.
 
Mcamreoon huyo, Omog ameifikisha Azam FC Robo Fainali ya Kombe la Kagame mjini Kigali kabla ya kutolewa na El Merreikh ya Sudan, iliyoibuka bingwa wa michuano hiyo mwaka huu. 
 
Wachezaji wa Azam waliotwa na kocha Mholanzi Mart Nooij kikosi cha Taifa Stars kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Morocco mjini Marakech Septemba 5, mwaka huu ni kipa Mwadini Ali, mabeki ni Said Morad, Shomari Kapombe, Aggrey Morris, viungo Erasto Nyoni, Himid Mao, Salum Abubakar na mshambuliaji John Bocco. 
 
Wataingia kambini Agosti 31, mwaka huu mchana katika hoteli ya Accomondia mjini Dar es Salaam.
 
Azam FC inatarajiwa kukutana na wapinzani wao katika mbio za ubingwa msimu uliopita, Yanga SC kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, Septemba 13, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
Aidha, mabingwa hao wataanza kutetea taji lao la Ligi Kuu kwa kumenyana na Polisi Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam Septemba 20, mwaka huu

chanzo: bin zubeiry

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.