Mwaikimba ni miongoni mwa wachezaji wakongwe kwenye Ligi Kuu Bara. Aliwahi kuichezea Yanga kwa mafanikio makubwa, Tanzania Prisons, Moro United na Ashanti. Amecheza ligi hiyo zaidi ya misimu 10.
Mwaikimba amebakiza mkataba wa miezi sita Azam FC na anaweza kufanya mazungumzo na klabu yoyote lakini Azam imesema haitaki kumuacha.
“Mwaikimba bado ni mchezaji wetu na ana mkataba na Azam, hivyo hatuwezi kumzungumzia sana kwa sasa ila bado tunamhitaji na ataendelea kuwa mchezaji wa Azam,” alisema Nassor.
CHANZO: SALEH JEMBE
0 Maoni:
Post a Comment