Azam FC imefanya usajili wa wachezaji wawili tu katika dirisha dogo, ambao beki wa kati Serge Wawa Pascal, raia wa Ivory Coast aliyekuwa anacheza El Merreikh ya Sudan na kiungo Amri Kiemba aliyesajiliwa kwa mkopo kutoka Simba SC.
Pamoja na hayo, mabingwa hao wa Tanzania Bara wamemchukua kocha Mganda, George ‘Best’ Nsimbe kuziba pengo la Muingereza, Kali Ongala aliyejiuzulu baada ya mechi sita.
Azam FC imeonyesha iko vizuri chini ya benchi jipya la ufundi, linaloongozwa na kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog baada ya jana kuwafunga vinara wa Ligi Kuu, Mtibwa Sugar mabao 3-1.
0 Maoni:
Post a Comment