Katika mchezo huo wa kirafiki uliochezwa katika uwanja wa azam complex, ikiwa ni mara ya kwanza kwa azam fc kucheza usiku katika uwanja huo, ulishuhudiwa na mashabiki wa wastani.
Azam fc ndio walikuwa wa mwanzo kupata goli, lililofungwa na Didier Kavumbagu, baada ya kutokea rapsha katika langu la mtibwa na mpira kumkuta Kavumbagu aliyekwamisha mpira nyavuni.
Goli la mtibwa sugar lilifungwa na Mussa Hassan Mgosi kwa mkwaju wa penati, huku goli la mwisho la azam fc lilifungwa na Khamis Mcha na kupelekea mchezo kumalizika kwa azam fc kuibuka na ushindi wa goli 3-1.
Azam fc wanataraji kwenda Uganda wakati wowote ule kwa ajili ya michezo mingine ya kirafiki.
0 Maoni:
Post a Comment