Tuesday, July 21, 2015

ALLAN WANGA AFUNGA USAJILI WA AZAM FC

Posted By: kj - 3:21 PM

Share

& Comment

Mshambuliaji wa kimataifa wa Kenya Allan Wanga leo amesaini kandarasi ya kuitumikia Azam FC kwa miaka miwili, akiwa mchezaji wa mwisho wa kigeni kusajiliwa na Azam FC katika dairisha hili la usajili.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika ukurasa wa Azam FC katika facebook Allan Wanga aliyekuwa anitumikia El merekh ya Sudan amesain kandarasi ya miaka miwili.

"Mshambulizi wa timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars aliyekuwa anakipiga Al Merrikh Allan Wanga amesign mkataba wa miaka miwili kuichezea Azam FC mchana huu na kukamilisha idadi ya wachezaji saba wa kimatafa...." ilieleza taarifa ya Azam FC katika ukurasa wake wa Facebook.

Wanga ni mchezaji wa pili wa kugeni kusajiliwa Azam FC katika wachezaji 5 waliokuja kujaribu bahati yao ya kusajiliwa na Azam FC na kufikisha idadi ya wachezaji 7 wakigeni.

Wachezaji wa kigeni watakao vaa jezi za Azam FC msimu ujao ni Alla Wanga (Kenya) Migi (Rwanda), Majegwa (Uganda), Kavumbagu (Burundi), Tcheche, Bolue na Wawa (Ivory cost) 

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.