Thursday, October 29, 2015

AZAM WAICHAPA JKT RUVU, WASHIKA USUKANI WA LIGI KUU YA VODACOM

Posted By: kj - 7:22 PM

Share

& Comment

Kavumbagu na Farid Mussa Maliki wakishangilia goli la kwanza la AZam FC lililo fungwa na Kavumbagu
Mabingwa wa klabiu bingwa Afrika mashariki na kati Azam FC leo wamefanikiwa kuwashusha kileleni mabingwa wa ligi kuu ya vodacom Yanga SC baada ya leo kuibua na ushindi wa goli 4-2 mbele ya JKT Ruvu.

Katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Karume jijini Dar es salaam Azam FC waliuwanza mchezo kwa kasi na katika dakika ya kwanza Azam FC walikuwa teyari wameshafika langoni mwa JKT Ruvu.


Katika dakika ya 4 Dider Kavumbagu akicheza mchezo wake wa kwanza msimu huu aliiandikia Azam FC goli la kuongoza akimaliza pasi ya Michael Bolue aliyekuwa anaanza kwa mara ya pili msimu huu.


Wakati JKT Ruvu wakiwa wamebutwaa na goli hilo la kwanza, JOhn Bocco aliandikia Azam FC goli la pili katika dakika ya 7 ya mchezo.


Baada ya Bocco kuandika goli la pili Azam FC walianza kuweka mpira chini na kupunguza kasi ya mchezo huku wakitawala vilivyo katika eneo la kati ya uwanja.


Katika dakika ya 32 Najim Magulu alitumia vyema makosa ya mabeki wa Azam FC kuondosha mpira katika eneo la hatari la kuipatia JKT Ruvu goli lao la kwanza katika mchezo huo wa leo na kupelekea mchezo kwenda mapumziko Azam Fc wakiwa mbele kwa goli 2-1.


Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Azam FC wakimpumzihsa Kipre Bolue na nafasi yake ikachukuliwa na Himid Mao.


Katika dakika 59 JKT Ruvu walipoteza nafasi ya wazi ya kujiandikia goli la pili kufuatia washambuliaji wa JKT Ruvu kushindwa kuweka mpira kimiani wakati wamebaki na nyavu na huku wakiwa wa wili dhidi ya beki mmoja wa Azam FC.


Shomari Kapombe katika dakika ya 60 aliangushwa katika eneo la hatari na mwamuzi kizawadia Azam FC penati iliyozaa goli la tatu kwa Azam FC iliyo pigwa na John Bocco.


Kuingi kwa goli hilo Azam FC walijaribu kupunguza kasi ya mchezo kitendo ambacho JKT Ruvu hawakuliwafiki na kuendeleza kasi ya kusaka goli.


Katika dakika ya 69 JKT Ruvu waliandika goli la pili kupitia kwa Emanuel Pius na kupeleka Azam FC kuanza kusaka goli la kumaliza mchezo huku JKT Ruvu wakisaka goli la kusawazisha.


Katika dakika za nyongeza mtokea benchi Kipre Tcheche aliiandikia Azam FC goli la 4 na kupeleka mchezo kumalizika kwa Azam FC wakiibuka na ushindi wa goli 4-2.


Katika ,mchezo mwingine wa ligi kuu ya vodacom uliochezwa katika uwanja wa Sokoine Mbeya Tanzania Prisons wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya African Sports.


Goli hilo pekee la Tanzania Prisons lilifungwa na Said Mkopi kwa mkwaju wa penati katika kipindi cha kwanza.



MATOKEO YA MICHEZO YA LEO

TANZANIA PRISONS 1-0 AFRICAN SPORT
JKT RUVU 2-4 AZAM FC



MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM BAADA YA MICHEZO YA LEO

RnTimuPWDLFAGdPts
1Azam FC87101551022
2YANGA86202051520
3MTIBWA SUGAR861184419
4SIMBA SC860294518
5STAND UNITED9513104616
6T. PRISONS951388016
7MWADUI FC9432106415
8TOTO AFRICANS934267-113
9MGAMBO SHOOTING932468-211
10MAJIMAJI FC932458-311
11MBEYA CITY922578-18
12NDANDA FC814346-27
13Coastal Union913517-66
14KAGERA SUGAR9126211-95
15AFRICAN SPORT810719-83
16JKT RUVU9027416-122

0 Maoni:

Post a Comment

Copyright © CHAMA LANGU NI AZAM FC™ is a registered trademark.

Designed by Templateism. Hosted on Blogger Platform.